Mbunge wa Wilaya ya Iganga Grace Hailat Kaudha Magumba ameaga dunia.
Kaudha mwenye umri wa miaka 31, alifariki katika Hospitali ya Jiji la Kampala huko Kawempe, Kampala Jumamosi saa nane usiku. Alikuwa anaujauzito wa miezi mitano.
Kwa mujibu wa gazeti la Monitor Chris Obore, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Umma wa ofisi za Bunge amethibitisha hilo.
“Spika wa Bunge la Uganda Rebecca Kadaga anasikitika kutangaza kifo cha Mbunge wa Wilaya Igunga Kaudha Grace Hailat ambacho kimetokea jana usiku,” amesema Jumamosi.
“Tunatuma salamu za rambirambi zetu kwa watu wa Busoga, wabunge na nchi nzima kwa kumpoteza kiongozi huyu. Maandalizi ya maziko yatatangazwa hapo baadae,” Obore alisema.
Lakini gazeti la Daily Monitor limesema limepata taarifa kuwa marehemu atazikwa siku ya Jumamosi, Julai 8, saa kumi jioni katika kijiji cha Magogo, Iganga.
Matarisho ya maziko yatafanyika huko katika shule ya msingi ya manispaa ya Iganga.

Tupia Comments: