SERIKALI imemsomea Mashtaka saba Mwenyekiti wa Quality Group Yusuf Manji na wenzake watatu yakiwamo ya Uhujumu uchumi na usalama wa nchi
Kesi walisomewa Kwenye Hospitali ya Muhimbili Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete alipolazwa Mtuhumiwa namba moja Yusuph Manji Mbele ya Hakimu Mkazib wa mahakama ya Kisutu Huruma Shahidi Wakili wa Serikali Kishenyi Mitalemwa aliwaomea washtakiwa mashataka yao.
Watuhumiwa wengine ni Pamoja na Abdala Sangey,  Deogratias Kisimba, na Tobias Fwele
Shtka la Kwanza Tarehe 30 Juni 2017 eneo la Changombe  Temeke Jijini Dar es Salaam walikutwa na Askari Polisi  wakiwa na mabunda 35 ya vitambaa yanayotumika kutengenea Sare  za Polisi zenye Thamani ya Milioni 192.5
Shitka la Pili watuhumiwa wote Tarehe 30 Juni walikutwa na Mabando Manane ya vitaambaa zinazotumika kutengeneza JWTZ
Kosa la Tatu  watuhumiwa walikuwa kukutwa na mihuri ya serikali washtakiwa wote  kwa pamoja tarehe 1 July  walikutwa na mihuri ya jeshi la Tanzania iliyoandikwa  "Mkuu wa Kikosi 121 Kikosi cha jeshi JWTZ "bila kuwa na uhalali kitendo kinachohatatisha usalama wa nchi
Kosa Nne watuhumiwa walikutwa na Mhuri wa Serikali walikutwa na muhuri wa JWTZ  yenye maandishi  Kamanda kikosi 834 KJ makutupola Dodoma bila kuwa na uhalali kitendo
Shtka la tano kukutwa na Mhuri wa Serikali wenye maneno "COMMANDING Oficcer 835 kj Mgambo P.O.BOX..."
Shtaka la sita kukutwa na mali inayozaniwa kupatikana isivyo halali Tarehe 1 Julai Changombe Plat namba SU 383 ambayo ilipatakan isivyo halali.
wahtakiwa Hawakuruhusiwa kujibu mashtaka hayo kwa sababu wanastakiwa kwa sheria ya Uhujumu Uchumi na usalama wa taifa.
Hakimu Shahidi amesma  Kwamba masuala hayo yasikilizwe kwenye Mahakama yenye mamlaka.
kesi hiyo itatajwa tena Tarehe 19 mwezi Julai  upelelezi wa Kesi haujakamilika.  

Tupia Comments: