MAMENEJA Sallam SK, Babu Tale, Mkubwa Fella, Wamesusa Wasanii wao Wanabanana WCB Kwa Diamond
Nakumbuka babu tale ndie mwanzilishi na meneja wa tip top connection kina madee, keisha, tunda, dogo janja etc... naona amekimbia lebo yake anabanana WCB.

Sallam nakumbuka ni meneja wa AY naona kamkimbia anabanana na WCB.

Mkubwa fella nakumbuka ni meneja wa Yamoto band, kina temba, chege etc naona nae amekimbia lebo yake anabanana WCB.

WCB patamu kuna safari za ulaya nyingi na Diamond ana hela ndefu wanyonyaji wote wameamua wakomae nae..

Ofisi ya WCB kila kitu ni gharama za Diamond.

Recruitment ya wasanii WCB ni diamond yaani diamond akisema chochote mameneja wanasema Yess boss

Sio majungu wadau ni maoni tu..

Kama hawa mameneja ni wazuri wanaupenda mziki wetu why wasiwamanage wasanii wao nao wawe kama diamond..

madee anapigia video posta barabarani siku ya jumapili maskini kuepuka msongamano.. meneja kakimbilia nyumba ndogo WCB.

Sallam, Babu tale na fella msikimbie nyumba zenu wasaniii wenu wanawahitaji muwakomboeeee...

Diamond ana familia inamtegemea sio kisa ameshatusua mkomae nae...Msimnyonyeeee sana

By Freshman/JF

Tupia Comments: