London, England. Kiungo wa West Ham, Jose Fonte amemsifu Mkenya, Victor Wanyama  kuwa ndiye kiungo bora kwenye Ligi Kuu England hivi sasa.

Mchezaji huyo raia wa Ureno aliwahi kucheza na Wanyama akiwa Southampton kati ya mwaka 2013 na 2016 pia aliwahi kufanya kazi na kocha wa Spurs, Mauricio Pochettino kwenye klabu za England.

Wanyama alicheza dakika 73 wakati Spurs iliponyukwa bao 1-0 dhidi ya West Ham kwenye uwanja wa London wakati wa mchezo wa Ligi Kuu mwishoni mwa wiki iliyopita.

Raia huyo wa Kenya amecheza michezo 33 ya Ligi Kuu akiwa na Spurs.  Pia, amefanikiwa kufunga mabao mawili tangu aliojiunga na Club hiyo akitokea Southampton Juni mwaka jana.

Tupia Comments: