Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  imetangaza muhtasari wa muelekeo wa bajeti kwa mwaka wa Fedha  2017-2018 kwa  mara ya kwanza kufikia Shilling Trilion 1,081.4 ambapo  ikitengemea makusanyo ya kodi ya  ndani ya nchi.
Ameyasema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Waziri wa Fedha na Mipango Dr.Khalid Salum Mohamed amesema muelekeo wa bajeti ya serikali kwa mwaka wa Fedha utatengemea  vyanzo vyake vya ndani vya mapato vinavyokusanywa  na taasisi za kodi nchini,mamlaka ya kodi TRA pamoja na bodi ya mapato ZRB.
Amesema taasisi hizo ambapo TRA inatarajiwa kukusanya  jumla ya shilling Billion 258.7 wakati bodi ya mapato ZRB inatarajiwa kukusanya Shilling Billion 347.3  kwa mwaka.
Alifahamisha  kuwa hii ni mara ya kwanza kwa bajeti ya serikali kufika katika kiwango hicho cha Fedha ambapo  miaka 2016-2017  ilifika Shilling Billion 841.5 kwa mwaka ambapo  bajeti ya mwaka huu haitatengemea  Fedha za wahisani na washirika wa maendeleo.
Mapema dk.Salum amevitaja  vipaumbele  vya serikali  ni pamoja na kuimarisha huduma za kijamii ikiwemo afya,elimu pamoja na miundo mbinu ya ujenzi wa barabara hadi vijijini.
Hata hivyo  amesema miradi ya ujenzi wa miundo mbinu imepewa kipaumbele  katika  kuingiza mapato ikiwemo kukamilika kwa jengo la abiri katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume,Bandari mpya ya mpiga duri huko Maruhubi

Tupia Comments: