Siku moja baada ya Rais Magufuli kuzuru kituo cha shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Nakuagiza kupitiwa upya mkataba wa uliongiwa baina ya shirika hilo na kampuni ya kichina ya Startimes, Basi Mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa Facebook ameandika hivi...

 "Nasikia Rais kaagiza kuhusu Mkataba wa StarTimes na TBC. Mwaka 2011 tulipata kuazimia Hivi;

"7.2.10 Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mkataba baina ya Shirika la Utangazaji Tanzania ( TBC) na Star Times International Communication una mapungufu kadhaa ya kisheria na ambayo yamebainishwa na Mkaguzi wa Hesabu wa TBC baada ya kuchambua Mkataba na Taarifa ya Hoja za Ukaguzi,na kwa kuwa mapungufu hayo yanaweza kuwa na athari katika utendaji wa TBC kwa siku zijazo , kwa hiyo basi Kamati inapendekeza kuwa, Serikali iupitie upya Mkataba huo ili kuainisha maeneo ya maboresho, aidha Serikali ifanye utaratibu wa kuangalia namna nzuri ya kutoa fedha kwa uendeshaji wa TBC ili kiwe chombo cha utangazaji wa Umma chenye kujiendesha kwa uhuru na kwa maslahi ya Umma."

Tupia Comments: