Vijana wameshauriwa kuchangamkia fursa za mikopo inayotolewa kuwawezasha kwa ajili ya shughuli za kijasiriamali ili kujikwamua na hali ngumu ya uchumi.
Akizungumza katika mafunzo kwa  wajasiriamali Vijana Mkurugenzi Ujasiriamali Idara ya Uwezeshaji Zanzibar Zeana Hamad Kassim amesema  kwamba mikopo hiyo inatolewa kwa lengo la kuwezesha vijana  kuweza kujiajiri ili  kupunguza tatizo la ajira Zanzibar.
Amesema  serikali inafanya jitahada mbalimbali ikiwemo utoaji wa mikopo kwa vikundi vya wajasiriamali  vijana  ili kupunguza idadi kubwa ya vijana  wasio na ajira  ambapo  taarifa zinaonesha  vijana wamebadilika  mtazamo  wa kutengemea ajira serikalini  na  kujikita katika ujasiriamali ili kujiwezesha kiuchumi.
Wamesema licha ya kuwa na muamko wa kushiriki katika shughuli mbalimbali ikiwemo za ujasiriamali ili kujikwamua na hali ngumu ya uchumi lakini bado  wanakabiliwa na ukosefu wa elimu ya ujasiriamali pamoja na ukosefu wa masoko ya kuuzia bidhaa wanazozizalisha hali inayopelekea kuvunjia moyo kwa kile wanachokifanya hivyo serikali kuliangalia kwa kina suala hili na sio kuwa wezesha tu bali hada masoko kuwatafutia kwa wakati.
Mafunzo hayo  ya siku moja yaliyoandaliwa na Jumuiya ya vijana ZAFAYCO yanalengo la kutoa hamasa kwa vijana juu ya umuhimu wa kujiajiri wenyewe katika Nyanja za maendeleo.

Tupia Comments: