Wizara ya elimu na Mafunzo ya amali Zanzibar  imesema kutokana na uharibifu mkubwa wa majengo  ya skuli Unguja na Pemba uliosababishwa na mvua zinazoendelea,  Serikali kwa makusudi itachukua juhudi za kuyafanyia  matengenezo majengo hayo ili wanafunzi kuwa katika mazingira salama.
Akizungumza na Zanzibar24, Mkurugenzi  Idara ya Elimu Sekondari Asya Iddi Issa amesema skuli nyingi unguja na pemba zinahitaji kufanyiwa matengenezo  yaharaka kutokana skuli hizo  kuingiliwa na maji ya mvua na kusababisha athari  ikiwemo kuta za skuli kufanya nyufa, kubomoka kwa vyoo,kuvuja kwa mapaa na kuharibika kwa mazingira ya maeneo ya skuli.
Amezitaja miongoni mwa skuli za unguja zilizopata athari mbalimbali kutokana na mvua ni Kibuyuni, Zingwezingwe, Bwejuu, Kajengwa, Miwaleni, Kizimkazi mkunguni, Miwani, Mchangani, Koani, Fuoni chunga, Lumumba, Ben-bella, Kidongo chekundu,  Nyerere, Jang’ombe   na   Muembe ladu na kutoa wito kwa wananchi na wadau mbalimbali  kutoa msaada  ili kuwasaidia watoto kusoma katika mazingira bora.

Tupia Comments: