MGANGA Mkuu wa Hospitali ya Mkoa ya Abdulla Mzee Mkoani Pemba, Dk. Haji Mwita Haji, akizungumza kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa vya mafunzo ya upasuaji mdogo kwa ajili ya wanaovunjika mifupa, kutoka hospitali ya Wuxi no 2 ya watu wa China, ambapo vifaa hivyo kwa Afrika Mashiriki pekee, vipo hospitalini hapo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

KIONGOZI mkuu wa madaktari wa kichina waliopo hospitali ya Mkoa ya Abdulla Mzee Mkoani Pemba, akizungumza kwenye hafla kukabidhiwa vifaa vya mafunzo ya upasuaji mdogo, kwa ajili ya wanaovunjika mifupa, kutoka hospitali ya Wuxi no 2 ya watu wa China, ambapo vifaa hivyo kwa Afrika Mashiriki, vipo hospitali hiyo pekee, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

KULIA ni rais wa hospitali ya Wuxi no 2 ya watu wa China, Dk. Cao Yue Zing akimkabidhi mwakilishi wa wizara ya afya Pemba Dk. Ali Omar Mbarawa vifaa vya kisasa, kwa ajili ya watu wanaovunjika, kwa ajili ya Hospitali ya Mkoa ya Abdulla Mzee Mkoani Pemba, ambapo vifaa hivyo kwa Afrika Mashiriki, vipo hospitali hiyo pekee, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

KULIA ni rais wa hospitali ya Wuxi no 2 ya watu wa China, Dk. Cao Yue Zing akimkabidhi mwakilishi wa wizara ya afya Pemba Dk. Ali Omar Mbarawa vifaa vya kisasa, kwa ajili ya watu wanaovunjika, kwa ajili ya Hospitali ya Mkoa ya Abdulla Mzee Mkoani Pemba, ambapo vifaa hivyo kwa Afrika Mashiriki, vipo hospitali hiyo pekee, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

MADAKTARI kutoka China, na wale wanaofanya kazi zao hospitali ya Mkoa ya Abdulla Mzee Mkoani Pemba, pamoja na watendaji wa wizara ya afya, wakiwa kwenye picha ya pamoja, baada ya kumaliza hafla ya kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya operesheni mdogo kwa wanaovunjika mifupa, na kutumia hospitali hiyo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

MADAKTARI kutoka China wanaofanyakazi zao za matibabu, Hospitali ya Mkoa ya Abdulla Mazee Mkoani Pemba, wakiwa tayari kushuhudia uzinduzi wa kituo cha mafunzo ya mpango wa upasuaji mdogo kwa ajili ya wananchi wanaovunjika, ambapo tayari nchi hiyo, imeshatoa vifaa ambavyo kwa Afrika Mashariki vinapatikana kisiwani Pemba pekee, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

KIONGOZI wa wizara ya afya Pemba kushoto Dk. Ali Omar Mbarawa, akiwa na rais wa hospitali ya Wuxi no 2 ya watu wa China, Cao Yue Zing wakiondoa kitambaa kuashiria kuzindua kituo cha mafunzo cha mpango wa upasuaji mdogo, kwa wanaovunjika mifupa, kwa wanaotumia Hospitali ya Mkoa ya Abdulla Mazee Mkoani Pemba, ambapo vifaa hivyo kwa Afrika Mashiriki, vipo hospitali hiyo pekee, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

VIFAA vya kisasa vyenye thamani ya shilingi milioni 60, vilivyotolewa na rais wa hospitali ya Wuxi no 2 ya watu wa China, Cao Yue Zing, ambapo vifaa hivyo vitaepusha mtu alievunjika kufanyiwa opereshehi mkubwa, kabla ya kutibiwa au kutiwa vyuma, ambapo vifaa hivyo kwa sasa ndani ya Afrika Mashariki, vipo kwenye hospitali hiyo ya Mkoa ya Abdulla Mazee Mkoani Pemba pekee, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

Tupia Comments: