Serikali ya Tanzania imeliagiza shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu Maendeleo (UNDP) kumuondoa mkurugenzi mkuu mwakilishi wa shirika hilo Tanzania kumuondoa kutoka nchini humo.
Tanzania imesema Bi Awa Dabo hajakuwa na maelewano mazuri na baadhi ya watumishi wenzake pamoja na wasimamizi wa shirika hilo.
Taarifa kutoka wizara ya mambo ya nje ya Tanzania imesema hilo limechangia "kuzorotesha utendaji wa shirika hilo nchini (Tanzania) na kupunguza kasi ya kuleta maendeleo kwa Watanzania endapo hatua za haraka hazingechukuliwa."
Serikali ya Tanzania kupitia wizara hiyo imetoa wito kwa UNDP kuwakumbusha watumishi wake kuwa "kipaumbele chao ni kufanya kazi na Serikali ili kufikia maendeleo yaliyoainishwa kwenye Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025, Mpango wa Maendeleo wa Miaka mitano na Malengo ya Maendeleo Endelevu ambayo yamefafanuliwa katika Agenda ya mwaka 2030."

Tupia Comments: